Ticker

6/recent/ticker-posts

KWA NINI DOLA INASHUKA?

                                     


KWA NINI DOLA INASHUKA?

 Ukienda benki leo ( 12 Disemba 2024), Utaambiwa ukiwa na dola Moja ya marekani ( usd), utapewa fedha ya Tanzania 2375.

Kama utakuwa mfuatiliaji wa namna dola ya marekani inavyokwenda utagundua kuwa dola imeshuka kwa kasi ukilinganisha na  mwaka jana.

Kumekuwa na maswali mengi "Je uchumi wetu umeshuka?, Uchumi wetu umepanda?, Je fedha yetu imeanguka au imeimarika?, Kuna faida yoyote kibiashara au hasara?,

Je dola ikishuka kuna athari yoyote kwenye uchumi wetu?, Je serikali inaweza kuratibu kupanda na kushuka kwa dola?,

Kwanza kwanini ishuke sasa hivi na sio mwaka jana?, Vipi itaendelea kushuka tena ama itapanda?".

Maswali kama haya na mengine mengi watu kadha wa kadha wamekuwa wakiuliza.

Kabla hatujaanza kuwajibu nadhani turudi nyuma kidogo.

 

UTANGULIZI.

Kama tulivyojifunza katika makala za nyuma kuhusu fedha. Ni kipindi cha mwisho wa vita kuu ya pili ya dunia mwaka 1944. Nchi 44 zilikaa ( Bretton Woods Agreement) na kukubaliana dola ya marekani itumike kama pesa ya biashara kimataifa na ndio mwanzo wa kuanzishwa benki ya dunia na shirika la fedha duniani( World bank and International Monitary Fund).Kuanzia hapo, basi dola ya Marekani ( usd) ilianza kutumika kama fedha ya kibiashara ya dunia ( world trade currency) na ikapalekea benki kuu za nchi tofauti tofauti kuanza kuhifadhi dola ( world reserve currency) ili ziweze kuitumia kuuza na kununua bidhaa kwa mfumo wa kibenki wa kimaghalibi yani ( Swift sytem) .

Kulingana na uhitaji huu wa dola basi fedha hii ilikuwa kama bihaa zigine. Moja kati ya sheria kuu ya uchumi , inasema kwamba kama bidhaa ikiwa nyingi na uhitaji ni mchache basi thamani ya ile bidhaa inashuka na kama bidhaa ikiwa chache na uhitaji mkubwa thamani ya ile bidhaa inapanda ( demand and supply law).

Kumbe sababu kubwa inayofanya bidhaa ( dola ) ipande ama kushuka ni  uhitaji wake ( demand) ukilinganisha na upatikanaji wake ( supply). Kwakua uthamani wa fedha hupimwa kwa kulinganishwa na dola. Kumbe dola ikipanda ukilinganisha na fedha ya nchi husika basi tunasema ile fedha imepungua thamani ukilinganisha na dola. Hali kadhalika dola ikishuka ( kama ilivotokea sasa) ukilinganisha na fedha ya Tanzania basi tunasema fedha ya Tanzania imepanda thamani kulinganisha na dola ya Marekani.

 

Baada ya kupata utangulizi basi twende pamoja kwenye uhalisia na ukweli hasa wa mambo.

 

KWANINI DOLA IMESHUKA THAMANI ?

 

Ili tuweze kulijibu swali hili kwanza inabidi tuwe na taswira mbili kwanza ni taswira ya kidunia pili taswira ya nchini kwetu Tanzania.

 

Tukianza na kidunia, Katika utangulizi tulisema dola ni kama bidhaa ( financial instrument), Kuna namna ambavyo mathalani hisa hupanda  ama kushuka thamani kwasababu wawekezaji wamepoteza imani ,ama imani imeongezeka kwenye hisa husika. Hii kitaalamu huitwa investors confidence. Kuna sababu kadhaa kidunia ambazo zimepelekea dola kushuka thamani .

1. Kupungua kwa imani ya dola kwa wawekezaji duniani

                  
        
Imani ya mataifa tofauti tofauti inapungua kulingana na sababu tofauti tofauti zikiwa ni pamoja na

A) sera na deplomasia ya Marekani ,

Mfano Marekani ilizuia fedha za Urusi zaidi ya dola billioni 800 kwa sababu ya uvamizi Ukraini. Hii ilikuwa kinyume na sheria za fedha za kimataifa. Hivyo nchi nyingine zinaona Marekani inaweza kufanya  hivyo kwa nchi yoyote inayopingana nae kisera, hasa kwa kuiwekea nchi husiks  vikwazo mfano ni Irani,bUrusi, Venezuela na Zimbambwe( weponizing of the currency).Ili kuidumaza kiuchumi

 

B) Uchaguzi wa Marekani

Baada ya raisi mteule  Donald Trump kushinda Uchaguzi wa Marekani. Kumekuwa na matamshi ya kuongeza kodi ya 100% kwa magari ya umeme ( Electric Vehicles) kutoka China ama kodi 10% kwa bidhaa kutoka nchi  zote duniani. Jambo hili linafanya nchi nyingine zipunguze imani na dola ya Marekani.

 

Hizi sababu zinapelekea uhitaji wa dola upungue. Ukipungua dola inakuwa nyingi kwenye mzunguko na hii inapelekea ishuke thamani.

 

2.Mabadiliko ya Uchumi wa Dunia ( Ukuwaji wa nchi za BRICS+)

                       


Baada ya vita kuu ya pili ya Dunia biashara zilifanyika kwa dola kwa zaidi ya 83%. Lakini kutokana na ukuaji wa Uchumi wa China na mataifa mengine,  biashra nyingi sasa zinafanyika kwa pesa ya China, India, Urusi, Japani na nchi nyingine.

Nchi za Brics+ hufanya baadhi ya biashara kwa kutumia pesa za nchi husika na ziko kweye mpango wa kuwa na fedha yake. Hii pia inapunguza uhitaji wa dola,  jambo linalofanya dola iwe nyingi kwenye mzunguko  na kuifanya izidi kushuka thamani.

 

3)Mazingira ya kiuchumi kidunia

Uchumi wa Dunia unategemeana( inter linked) baina ya nchi moja na nyingine.Hapa ntakupa mfano mdogo. Nchi ya Japani ndio nchi inayoongoza kwa watu kutunza fedha ( world no. 1 savers) na  wawekezaji wengi wa Kimarekani wamekuwa wakikopa fedha benki za Japani kwakua riba ni ndogo na kuwekeza Marekani. Hivyo wawekezaji huuza yeni ya Japani na kununua dola . Miezi kadhaa nyuma kutokana na matatizo ya kiuchumi, Benki kuu ya Japani iliamua  kuongeza riba( interest rate). Hii ilipelekea wawekezaji wengi wa Marekani kuuza hisa zao ili wanunue pesa ya Japani kurudisha mikopo ( market panic) halii hii inaongeza dola kwenye mzunguko na kuifanya ishuke thamani zaidi.

 

Hizi ni baadhi tu ya sababu za kidunia zinazopelekea Dola kushuka thamani.

 

KWANINI  SASA DOLA INASHUKA THAMANI NCHINI TANZANIA?

Kushuka kwa dola nchini haiwezi kuwa ni matokeo ya kushuka kwa dola kidunia peke yake, kwa sababu. Tukiangalia nchi zinazotuzunguka kama Kenya, Uganda, Zambia, Msumbiji  na Congo huko dola haijashuka na sehemu iliposhuka imeshuka kwa asilimia chache sana kulinganisha na nchini. Kumbe kipi kimefanyika nchini hadi dola ishuke na shilingi ya Tanzania ipande thamani?.

Kuna sababu nyingi ila sababu kubwa  ni

1. Sera za kifedha za benki kuu ya Tanzania  

                                    

Tulijifunza kwenye makala ya nyuma kuwa ili fedha iwe na nguvu( stable ) inabidi ipigwe tafu ( backed) na dhahabu. Benki kuu ya Tanzania imekuwa ikinunua dhahabu kwa muda sasa,hii imeifanya shilingi kuongezeka thamani na kuwa na nguvu.

2. Kupunguza uhitaji wa dola.

Kwa muda sasa benki kuu ilikataza matumizi au malipo ya dola kwenye biashara za ndani. Hali hii imepelekea ongezeko la dola na kufanya ishuke thamani.

 

3. Kuongezeka kwa upatikanaji wa dola.

Kuna njia tofauti tofauti ambazo nchi hupata dola ama fedha za kigeni . Njia hizi ni kama kuuza bidhaa nje, utalii, mikopo na misaada. Kumekuwa na ongezeko kubwa la sekta ya utalii hali ambayo imeongeza upatikanaji wa fedhs za  kigeni na kulingana na Sera za benki kuu watalii hawa wanatakiwa walipe malipo kwa shilingi ya Tanzania hivyo dola zinabaki benki.Hili linaongeza upatikanaji wa dola zaidi na kuifanya ishuke thamani.

FAIDA NA HASARA ZA KIUCHUMI ZITOKANAZO DOLA KUSHUKA THAMANI

Kushuka ama kupanda kwa dola ni kama pande mbili za sarafu kuna faida na hasara zake. Siku zote kiuchumi huwa tunafanya kitu ambacho faida ni kubwa kuliko hasara.

 

HASARA

Kwa nchi ambayo uchumi wake hutegemea zaidi kupeleka bidhaa nje ( export) mfano China au Ujerumani hupendelea zaidi dola ipande thamani zaidi,ili bidhaa zake ziwe bei chini na kuvutia wateja na wawekezaji zaidi.

Kushuka kwa dola kuta athiri biashara zote zinazopelekwa nje ya nchi kama bidhaa za uvuvi, kilimo au madini. Kwakuwa watu hawa watapata faida kidogo ukilinganisha na awali na bidhaa husika zitakuwa na bei kubwa kwenye soko la dunia hivyo kuwa na ushindani mdogo. ( low compititive advantage)

 

FAIDA

Waswahili wanasema kifo cha panzi furaha kwa kunguru. Kwa zile biashara zinazoagizwa kutoka nje kama bidhaa kutoka China, magari kitoka Japan ama mashine kitoka Ujerumani.  Hawa wote watapata faida zaidi kwakua watatumia pesa kidogo kununua mzigo ule ule .Kwa kuwa bidhaa nyingi za uzalishaji ( capital goods) hutoka nje ya Nchi .Basi, hii itasaidia ukuaji wa uchumi na kupunguza mfumuko wa bei , sababu ya kupungua garama za uzalishaji ( decresse in cost push inflation.

 JE DOLA ITAENDELEA KUSHUKA? AU ITAPANDA


Kwa mwenendo wa sera za Marekani . Ni mapema sana kujua kitakachotokea baada ya kuapishwa Donald Trump. Japoluwa kwa sasa hadi mwezi January kuna muenendo mkubwa wa dola kushuka thamani . 

Ila kwakua Trump ni kiongozi anae amini zaidi katika kuimarisha dola  na katika uwekezaji zaidi , huku akiongelea mfumuko wa bei wa Marekani kuna uwezekano mkubwa wa benki kuu ya Marekani kuongeza riba zaidi . Hili  Kwa  mataifa makubwa zaidi  kama Chins , India ama Japani inaweza pelekea Dola kupanda kwenye nchi zao ama kidunia. Ila kwa mataifa kama ya Africa itategemea sera za nchi . Kama Sera za benki kuu zitazidi kupunguza uhitaji wa dola basi . Dola itaendelea kushuka zaidi kwa Tanzania . Ikumbukwe kwamba leo hii tunaongelea kushuka kwa dola Tanzania lakini Zambia , Msumbiji, Uganda na Congo kwao dola imepanda thamani , haijshuka. Kwa sababu ya Sera za benki kuu yao

 

KWA UJUMLA.

kama nchi inaagiza vitu kutoka nje zaidi ya inavyopeleka nje ya nchi( negative balance of payments), Nchii itanufaika na kushuka thamani kwa dola. Na kama nchi inapelekea bidhaa nje zaidi,  kuliko inavyo ingiza nchini( positive balance of payments), Nchii hii itanufaika zaidi na kupanda thamani kwa dola.

 

Kwa kuhitimisha kabisa. Tuzidi kutumia fursa hizi za kushuka kwa dola kuji imarisha kwa uchumi binafsi.

Nashukuru kwa kuwa pamoja nami katika makala hii  na Mungu wa Mbinguni akubariki.

Asante sana.

Makala hii imeandaliwa na

Erick Muhini ( Agro Economist)

Post a Comment

18 Comments

  1. Maelezo mazuri japokuwa naona vyombo vingi vinaripoti kuwa dola inazidi shuka kwenye nchi nyingi hata kwenye hizo nchi ulizotaja zinazozunguka tanzania kama sikosei.

    ReplyDelete
    Replies
    1. There are some of the contries where dollar is getting stronger and some where it's not . For example in Zambia dollar is getting stronger against Zambian Kwacha

      Delete
    2. Dola Ina panda na kushuka kila siku , ungejaribu kuangalia muenendo wake kwa mwezi huu wa Desemba . Tunashukuru kwa kusoma Makala🙏🏿

      Delete
  2. Ni jambo jema Kama umejifunza . Kukiwa na kitu kinahitaji ufafanuzi karib sana Chief

    ReplyDelete
  3. Mnakaa kimya sana agroottomans ,,Kubabake Trump kazi anayoo 😀😀😀😀😀😀😀nacheka kama mazuri

    ReplyDelete
    Replies
    1. Tutajitaidi tusiwe kimya hivi . Kuhusu Trump Ngoja akianza io January tuone mzee

      Delete
  4. Replies
    1. Bila shida kabisa unaweza ku copy pia uka share na Marafiki mkuu

      Delete
  5. Pia Kama kuna kitu ungependa kujifunza kuhusu Uchumi, kilimo ama biashara karibu

    ReplyDelete
  6. Makala nzuri sana,, vijana ni frusa kwetu

    ReplyDelete
  7. Asante sana . Hii ni kweli ni fursa

    ReplyDelete