HEAT STRESS IN A DAIRY COWS
(Shinikizo la joto)
Hili ni moja ya tatizo
kubwa ambalo hutokea kwa ngombe wengi, hasa wakati wa kipindi cha joto. Tatizo
hili mara nyingi huwa linamfanya ngombe kuwa na joto kubwa la mwili
ukilinganisha na joto lake la kawaida. Tatizo hili hupelekea ngombe kupunguza
uzalishaji wake kwa mfano ngombe atapunguza kiasi cha maziwa ambacho anatakiwa
kutoa kila siku, pia inapunguza uwezo wake wa kuzaa (fertility) kwa ngombe
husika.
Leo
tutaangalia na kuongelea upande wa kuzalisha maziwa
Hapa
nisikilize kwa makini nataka kukuambia kwanini ngombe atapunguza uzalishaji wa
maziwa akipata na heat stress…..
Ni kitu kidogo tu na cha
kawaida sana. Pale ambapo tu joto linaongezeka ndipo hapo hapo ngombe
anapunguza ulaji wa chakula na anapopunguza ulaji wa chakula ndipo tunapata kitu
kinaitwa low forage intake, yaan lishe duni kwa ngombe ambapo hii itapelekea
kwenye rumeni ya ngombe kuwa na hali ya acid nyingi na kupunguza fat contents
of milk ambapo moja kwa moja itapelekea
kupunguza uzalishaji wa maziwa. Kwa sababu, hizo fat content of milk ndo zinazohusika
moja kwa moja kwenye uzalishaji maziwa ya ngombe
Sasa
twende pamoja tuone nini kinatakiwa kifanyike ili kuweza kuwaondoa ngombe na
hili hali ya heat stress………
Vitu
unavyotakiwa kuvifanya ili usiingie kwenye athari la ongezeko la joto ni kama
ifuatavyo
·
Kuwaongezea kiwango cha maji wanayokunywa
kila siku. Hii ni muhimu sana kwa sababu maji yatapooza joto la mwili kwa
haraka sana hivyo ni muhimu sana kuwaongezea kiwango cha maji wanayokunywa. Hii
hufanyika vipi sasa? Waongeze vifaa vya kuwekea maji ya kunywa kwenye zizi lao,
kama wnaafuata maji ya kunywa umbali mrefu basi wapunguzie huo umbali maji yawe
karibu yao Zaidi.
·
Kuwe na tabia ya kuwanyunyuzia maji ngombe
wako kwenye miili hasaa wakati wa jua linapowaka hii itawasaidia ngombe kupooza
miili yao na kubaki na joto lao lile la kawaida. Hapa kuna vifaa maalum ambavyo
vinatumika kwa ajili ya kuwanyunyuzia maji.
·
Ujitahidi banda lako liwe na muingiliano
mkubwa wa hewa kwa sababu kama muingiliano utakuwa mdogo hii itapelekea hewa
iliopo ndani kuwa ya moto hivyo kufanya banda zima kuwa na joto na hivyo ngombe
watapandisha joto lao la mwili
·
Pia unashauriwa kuweka feni ndani ya zizi
lako kama mifugo yako haitoki nje kwa siku nzima. Feni hizi zinatakiwa kuwashwa
pale tu ambapo unaona joto limekuwa kali ndani ya zizi na hii hutokea mara nyingi
wakati wa mchana ambapo jua linawaka.
·
Epuka kuwafanyia chanjo za mara kwa mara
kipindi cha joto. Hii inamaanisha unatakiwa kuwa makini sana kipindi cha joto
ili kuwaepusha ngombe wako na magonjwa na kuwaepusha kwenye swala la kuwapa
chanjo za mara kwa mara. Kwa sababu chanjo zinapelekea joto la mwili kupanda.
·
Kitu kingine ni kuwa na mazoea ya kuwapima
joto la mwili mara moja kwa wiki ili kuona hali ya joto ya miili yao inavyoenda
na kujua kama njia ambazo unazitumia kushusha joto la mwili kama zinafanya
kazi.
·
Mwisho kabisa na ndicho cha umuhimu sana
kwa ajili ya kuzalisha maziwa ni swala la kubalance vyakula katika kipindi hiki
cha joto. Mwanzo kabisa tuliona kwamba mifugo itapunguza kula chakula wakati wa
kipindi hiki cha joto na kupelekea kupunguza uzalishaji wa maziwa ,hivyo basi
tukiweza kubalance vyakula kwenye kipindi hiki cha joto basi tutaepuka athari
ya kupungua kwa maziwa kwenye kipindi hiki cha joto. UNAWEZA KUJIULIZA SASA
HAPA TUNAFANYAJE…….Sikia ipo hivi kuna
vitu vitatu hapa vya umuhimu ambavyo tunaweza kufanya kwenye swala la chakula.
Kwanza kabisa
ujitahidi kwa wakati wa joto kuwapa mifugo chakula chenye quality ya juu kabisa
ile quality ya kwanza kabisa kama ni majani mabichi basi ujitahidi uwape yale
mazuri kabisa kwa sababu anakuwa amepunguza hamu ya kula kwa hiyo lazima tumpe
chakula kizuri sana ili aweze kula Sanaa. Na hapaa tutakuwa tumeipunguza ile
hali kuwa mifugo kuwa wanapata LOW FORAGE INTAKE ambayo tuliona mwanza kabisa
wa Makala hii. Hapa tunasema mifugo wanatakiwa kupata HIGH QUALITY FORAGE
Wapewe chakula cha
jamii ya nafaka, hii ni muhimu kwa sababu aina hii ya vyakula huwa na kazi ya
kuzalisha nguvu(ENERGY) mwilini, nguvu hiyo itatumika kwenye uzalishaji wa
maziwa kwa ngombe.
Mwisho ni inabidi
kufanya nyongeza ya fats content kwenye lishe yao ya kila siku. Kama tulivyoona
kwenye kipindi hiki cha joto kutakuwa na upungufu wa fats contents ambazo
zinahusika moja kwa moja kwenye uzalishaji wa maziwa. Kwahiyo ni muhimu sana
kufanya nyongeza ya fats kwenye lishe yao ya kila siku ili kufidia ule upungufu
ambao unatokea.
Kwakufanya
hayo yote lazima utaona matokeo kwenye mifugo yako hasa kwa wakati huo wa joto.
ASANTENI
NA KARIBUNI KUENDELEA KUFUATILIA UKARASA WETU NI MATUMAINI YETU MNAJIFUNZA
MENGI KUPITIA UKURASA HUU. KAMA UNATAKA KUJUA ZAIDI AU KUELEWA ZAIDI TUPIGIE
SIMU AU KUTUMA UJUMBE KWENYE MITANDAO YETU YA KIJAMII.
PIA
TUNAKARIBISHA MAONI NA MAPENDEKEZO MNATAKA TUONGELEE KITU GANI KWENYE MAKALA
ZIJAZO ILI MUENDELEE KUJIFUNZA ZAIDI.
0 Comments