1. Taarifa sahihi
Hakikisha una taarifa sahihi katika aina ya uwekezaji unaotaka kufanya . Taarifa sahihi hutegemea aina ya mtu ama watu waliokupa taarifa hizo . Anae kupa taarifa itafaa sana kama ni mtu ambaye aidha amewahi fanya uwekezaji huo ama utafiti wa kutosha kwa uwekezaji husika .Taarifa sahihi ndio chanzo cha kufanya biashara yako isimame . Katika kilimo huwa tunatumia bei za msim uliopita kujaribu kuangalia bei za msim ujao yaani kitaalam ( Cobweb Model) . Hii ni njia sahihi lakini inabid kulinganisha miaka kadhaa ya nyuma ya tabia za masoko, bei na mifumo ya serikali ili kuweza kufanya maaamuzi sahihi . Njia hii kitaalamu inaitwa (Trend analysis)

2. Mtaji
Mtaji si lazima uwe wa fedha . Unaweza kuwa na mtaji wa fedha, watu , ardhi, taarifa ama mawazo. Kulingana na sehemu ya mnyororo wa thamani unaotaka kuwekeza yani mathalani shambani, sokoni , usafirishaji ama uchakataji . Hakikisha una aina ya mtaji unaoitajika. Kama unahitaji kuwekeza kwenye masoko hakikisha una mtaji mkubwa wa taarifa za masoko. Kama unapenda kuwekeza kwenye kutoa huduma Kama semina, hakikisha una mtaji wa kutosha wa mawazo . Mfano kwa mtu anae taka kuwekeza shambani lazima awe na mtaji wa fedha, ardhi , watu na kadhalika . Ieleweke kuwa mtaji katika uwekezaji si fedha peke yake . Na wakati meingine unaweza kuwekeza bila kutumia fedha ( skills investment ). Ukubwa wa mtaji utasaidia mambo kadhaa.
a) ukubwa wa biashara utakayo ifanya
b) kiasi cha ukuwaji wa biashara yako
c) Jinsi unaweza kusimama pindi biashara yako imeanguka
d) Ukubwa ama udogo wa biashara yako na uwezo wa kupambana na misukosuko
Uwekezaji katika kilimo hasa shambaani unahitaji mtaji wa kutosha . Hakikisha kiwango cha uwekezaji ( scale of investment) inaendana na mtaji na muda ulionao.
3. Maarifa ( elimu)
Warren Buffet muwekezaji mkubwa ( investor of all time )zaidi duniani aliwahi kusema ivi " kama haujui kila kitu kuhusu biashara yako lazima biashara hiyo itakufa ". Wengi wanadhani ukishakuwa na mtaji tu unaweza kuwekeza kwenye kilimo. Kilimo ni uwekezaji ambao ni rahisi sana kupoteza mtaji wako wote . Hili linatokana na kuwa kilimo ni uwekezaji ambao kwa kiasi kikubwa hutegemea uhitaji na ugavi ( forces of supply and demand) . Kiuchumi kilimo hufananishwa na biashara huria ( perfect competitive market ). Swala hili hufanya bei za bidhaa za kilimo kubadilika mara kwa mara . Na kwakuwa kilimo hutegemea sana mabadiliko ya tabia ya nchi , uwekezaji huu unaitaji sana maarifa na elimu ya kutosha . Unaweza pata elimu hii kwa kujifunza katika semina na makala mbalimbali . Tumia muda mwingi kujifunza kabla haujaanza kufanya uwekezaji katika kilimo. Wengi wamekuwa wakikurupuka na wakijikuta wanapoteza pesa nyingi .
4. Uwezo5. Chagua eneo la kuwekeza
Tunashukuru kwa kupitia makala hii ubarikiwe usiache kufuatilia tovuti yetu kila siku
0 Comments